Saturday, 8 June 2019

MATUKIO KATIKA PICHA: DADA DETAH AKUTANA NA EKINGO

…..Dada tena akutana na Bw. Ekingo…….



Bw. Ekingo akimwangalia dada Detah kwa jicho la husda huku Dada Deta akiachia tabasamu kwa mbaaaali...Ilipendeza sanaaaaa

Sherehe za Idd zilimkutanisha Bw. Ekingo Ekingo na dada Detah, kwa kweli ilikuwa furaha sana kama picha zinavyoonesha…..

JAPHET TIBENDA MPIGA PICHA BORA 2018

…...Pale mpiga picha anapopigwa picha…. Bw, Jephet Tibenda akiwa kazini…. Hogera sanaaaaa

Timu ya SVSC imebarikiwa kuwa na vipaji bora kama wapiga picha. Kwa mwaka wa 2018 Bw. Japhet Tibenda alikuwa mpiga picha bora kama anavyoonekana
Mpiga picha bora akiandaa mtambo wake kabla ya kuingia kaazini

MICHAEL SIMBAULANGA MCHEZAJI MWENYE NIDHAMU SVSC 2018

Mwenyekiti SVSC akimkabidhi Bw. Michael Simbaulanga cheti cha nidhamu huku mwenyekiti mstaafu akishuhudia kwa karibu. Tunampongeza sana…..

Kila mwaka timu ya SVSC huchagua mchezaji mwenye nidhamu nje na ndani ya mchezo. Kwa mwaka 2018 Bw. Michael Simbaulanga amechaguliwa na kamati maalumu kwamba yeye ndiye mchezaji mwenye nidhamu kwa mwaka 2018. Tunampongeza sanaaaa.







MWENYEKITI SURVEY VETERANS AKIWAKARIBISHA WAGENI

Mwenyekiti  wa Survey Veterans akiwakaribisha wanachama na wapenzi wa SVSC katika hafla ya kupongezana na kusherehekea sikukuu ya Idd pili.

Baada ya mchezo kumalizika wapenzi na wanachama wa SVSC walikusanyika katika Bar ya Etina kwa ajili ya matukio mbalimbali 
Mkurugenzi Etina Bar and Restaurant Bw. Coster akiwakaribisha wapenzi na wanachama wa SVSC katika bar yake kwa ajili ya kusherehekea sikukuu\


TIMU ZENGWE YAILAZA TIMU BOMBA MAGOLI 5-2

Kikosi cha timu Zengwe kutoka kushoto waliochuchuma ni Samson Mwakei, Ramadhani, Musa Siwiti, Kasimu Ramia, Sparon Musa, Salum Mvule, Samweli Mbaga (golikipa), Mwandumbya, Michael simbaulanga, Hamis Gaga, Juma Ntalika (Chinga) na Frank Gasper. waliosimama kutoka kulia ni Chacha kibago, Ahmed shaweji, Emanuel Ekingo, Abdalla Kasim, Joseph Mtoimbamba, Ramadhani hamis, David Kiganga, Weston Kipangura, Kelvin Haule, Innocent Kuzengwa, Mwinyi Omary na Siasa.

Kama ilivyo ada inapofika sikukuu ya Idd pili. Timu ya Survey Veterans huadhimisha kwa mchezo wa kirafiki kati ya timu zinazounda Umoja huu ambayo ni Timu ya Mwl Bomba na Timu ya Mwl Msaidizi Adam Zengwe. kwa mwaka huu Timu bomba ilifungwa magili matano kwa moja.




Winga hatari, winga wa kuingia nazo…… Musa Siwiti akitimiza majukumu yake.





……….Hakuna goli hapa….. Golikipa hatari Mbaga akiokoa mpira wa kichwa uliopigwa na Benson Hagai ambao haukuzaa matunda…..

……..GOOOOOOOOHHHHHHHHH...…….. Kelvin Haule goli la pili baada ya kupiga faul iliyosababishwa na beki wa timu Bomba Idd Kaonenka baada ya kumchezea madhambi winga hatari Musa siwiti

…….Wengine walikuwa watazamaji tu  Mwenyekiti SVSC alicheza kwa dakika 15 tu akatolewa nje na timu yake baada ya kuonekana alikuwa anadhurura tu uwanjani.

>>>>>Hapa hupiti…. Hamad Shaweji akimdhibiti Peter Simon (Kitop) asilete madhara huku bilauri akimlinda kwa mbali

>>>>>Bunyabunya nao walikwepo japo hawakuwa na mdhara kabisa kwa timu pinzani

Mkwaju wa Weston Kipangule mwenye soksi za njano ulipanguliwa na golikipa wa timu Bomba

…...Hapa upiti Idd Ngaoneka akimkimbiza David Kiganga huku Frank Gaspar akimsaidia kwa nyuma.

Kelvin Haule akifunga goli la kwanza baada ya kupokea pasi kutoka kwa winga hatari Musa Siwiti hayuko pichani huku beki wa Timu Bomba joseph Mwasenga akiangalia kwa mbali.