Wednesday, 3 January 2018

SALAMU ZA MWAKA MPYA KUTOKA KWA MWENYEKITI WA SURVEY VETERANS




Heri ya mwaka mpya 2018 wana Survey Veterans Sports Club.
Mwaka 2017 tumeshauacha na changamoto zake la msingi ni kumshukuru Mungu Kwa uzima na afya njema alizotuzawadia hadi tunaweza fika na kufanya mazoezi/mechi pamoja na kutekeleza majukumu yetu ya kila siku.
Ki timu changamoto kubwa zilizojitokeza ni,
1) Kumekuwa na ongezeko la matokeo mabaya katika mechi tulizocheza kulinganisha na kipindi cha nyuma naomba Benchi zima la ufundi iliangalie hilo.
2) Kupitia uongozi kumekuwa na mapungufu sana ya ukusanyaji wa Ada za mwezi hili tutalirekebisha kuanzia kwetu sisi uongozi ili Mambo yaendelee vizuri.

Mwaka 2017 tumekuwa na mazuri mengi sana hasa kimechezo mbali mbali ya ndani na nje ya Dar, hatukukwama kusafiri,au kushiriki lolote lililokuwa linatupasa kushiriki, hatujakwama kujitunza Kwa maana ya vifaa pia na kusaidiana katika matatizo/mafanikio mbali mbali.
Katika hayo nawashukuru sana Kwa niaba ya Uongozi.
Vile vile nawapa pole sana wale waliopata misiba na matatizo mbali mbali sambamba na hilo nawapongeza wale wote waliofunga ndoa na waliopata mafanikio binafsi katika upambanaji wa kimaisha. PhD holders wanaongezeka sana. 👏🏾👏🏾👏🏾
2018 iko mbele yetu,Wazanzibari wanakuja pamoja na mengineyo naendelea kuwaomba ushirikiano wenu.
Mungu ibariki Tanzania.
Mungu ibariki SVSC.
Mwenyekiti SVSC.

0 comments:

Post a Comment