Saturday, 26 March 2016

SURVEY VETERANS KATIKA MAANDALIZI YA MWISHO KUELEKEA MASHINDANO YA MICHEZO YA PASAKA

SURVEY VETERANS KATIKA MAANDALIZI YA MWISHO KUELEKEA MASHINDANO YA MICHEZO YA PASAKA

Timu Zengwe kabla ya mchezo. Kutoka kulia waliochuchuma, Steven Nyenge, Kabambo jnr,Albart Sengo,Kipa hatari Ramadhani,Frank Gaspar. Waliosimama kutoka kushoto, Oscar Kobi, Adam Zengwe,PeterNgasa,B. Magadula,S. Kambabhe, Humphrey Machota,Innocent Mchaga,Carlos Mlinda, Peter Mweta, Dominic Mbwete na T. Bilauli


Timu ya SVSC ilikuwa na mechi ya kirafiki kati ya Timu Zengwe na Timu Bomba mchezo uliochezwa uwanja wa JKM Sports Park Kidongo chekundu. Timu hizi zilitoshana nguvu kwa kufungana magoli 3-3. Timu Zengwe ilisawazisha kipindi chapili kwa taabu sana baada ya kuelemewa toka mwanzo wa mchezo hadi mwisho. Timu Bomba itabidi wajilaumu baada ya kukosa magoli mengi kupitia mafowadi wao Kiganga na Sise ambao walipoteza umakini katika kuipatia timu yao magoli.


Peter Mweta kabla ya mchezo

Mashabiki wa Timu zengwe Richard Shukia na Machota

Mchaga kabla ya mchezo

0 comments:

Post a Comment